Zab. 80:9-14 Swahili Union Version (SUV)

9. Ulitengeneza nafasi mbele yake,Nao ukatia mizizi sana ukaijaza nchi.

10. Milima ilifunikwa kwa uvuli wake,Matawi yake ni kama mierezi ya Mungu.

11. Nao uliyaeneza matawi yake hata baharini,Na vichipukizi vyake hata kunako Mto.

12. Kwa nini umezibomoa kuta zake,Wakauchuma wote wapitao njiani?

13. Nguruwe wa msituni wanauharibu,Na hayawani wa kondeni wanautafuna.

14. Ee Mungu wa majeshi, tunakusihi, urudi,Utazame toka juu uone, uujilie mzabibu huu.

Zab. 80