Zab. 80:14-18 Swahili Union Version (SUV)

14. Ee Mungu wa majeshi, tunakusihi, urudi,Utazame toka juu uone, uujilie mzabibu huu.

15. Na mche ule ulioupandaKwa mkono wako wa kuume;Na tawi lile ulilolifanyaKuwa imara kwa nafsi yako.

16. Umechomwa moto; umekatwa;Kwa lawama ya uso wako wanapotea.

17. Mkono wako na uwe juu yakeMtu wa mkono wako wa kuume;Juu ya mwanadamu uliyemfanyaKuwa imara kwa nafsi yako;

18. Basi hatutakuacha kwa kurudi nyuma;Utuhuishe nasi tutaliitia jina lako.

Zab. 80