17. Wewe uliiweka mipaka yote ya dunia,Kaskazi na kusi Wewe ulizitengeneza.
18. Ee BWANA, uyakumbuke hayo, adui amelaumu,Na watu wapumbavu wamelidharau jina lako.
19. Usimpe mnyama mkali nafsi ya hua wako;Usiusahau milele uhai wa watu wako walioonewa.
20. Ulitafakari agano;Maana mahali penye giza katika nchiPamejaa makao ya ukatili.