7. Macho yao hutokeza kwa kunenepa,Wameipita kadiri ya mawazo ya mioyo yao.
8. Hudhihaki, husimulia mabaya,Husimulia udhalimu kana kwamba wako juu.
9. Wameweka kinywa chao mbinguni,Na ulimi wao hutanga-tanga duniani.
10. Kwa hiyo watu wake hugeuka huko,Na maji yaliyojaa humezwa nao.
11. Nao husema, Mungu ajuaje?Yako maarifa kwake aliye juu?
12. Fahamu, ndivyo walivyo wasio haki,Na kwa kustarehe sikuzote wamepata mali nyingi.
13. Hakika nimejisafisha moyo wangu bure,Nimenawa mikono yangu kwa kutokukosa.