15. Kama ningalisema, Nitasimulia kama hayo;Kumbe! Ningaliwadanganya kizazi cha wana wako.
16. Nami nalifikiri jinsi ya kufahamu hayo;Ikawa taabu machoni pangu;
17. Hata nilipoingia katika patakatifu pa Mungu,Nikautafakari mwisho wao.
18. Hakika Wewe huwaweka penye utelezi,Huwaangusha mpaka palipoharibika.
19. Namna gani wamekuwa ukiwa mara!Wametokomea na kutoweshwa kwa utisho.