Zab. 73:15-19 Swahili Union Version (SUV)

15. Kama ningalisema, Nitasimulia kama hayo;Kumbe! Ningaliwadanganya kizazi cha wana wako.

16. Nami nalifikiri jinsi ya kufahamu hayo;Ikawa taabu machoni pangu;

17. Hata nilipoingia katika patakatifu pa Mungu,Nikautafakari mwisho wao.

18. Hakika Wewe huwaweka penye utelezi,Huwaangusha mpaka palipoharibika.

19. Namna gani wamekuwa ukiwa mara!Wametokomea na kutoweshwa kwa utisho.

Zab. 73