Zab. 73:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli,Kwa hao walio safi mioyo yao.

2. Nami miguu yangu ilikuwa karibu na kupotoka,Hatua zangu zilikuwa karibu na kuteleza.

3. Maana naliwaonea wivu wenye kujivuna,Nilipoiona hali ya amani ya wasio haki.

Zab. 73