Zab. 71:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Nimekukimbilia Wewe, BWANA,Nisiaibike milele.

2. Kwa haki yako uniponye, uniopoe,Unitegee sikio lako, uniokoe.

3. Uwe kwangu mwamba wa makazi yangu,Nitakakokwenda sikuzote.Umeamuru niokolewe,Ndiwe genge langu na ngome yangu.

4. Ee Mungu wangu, uniopoe mkononi mwa mkorofi,Katika mkono wake mwovu, mdhalimu,

5. Maana ndiwe taraja langu, Ee Bwana MUNGU,Tumaini langu tokea ujana wangu.

6. Nimekutegemea Wewe tangu kuzaliwa,Ndiwe uliyenitoa tumboni mwa mama yangu,Ninakusifu Wewe daima.

Zab. 71