Zab. 7:13-16 Swahili Union Version (SUV)

13. Naye amemtengenezea silaha za kufisha,Akifanya mishale yake kuwa ya moto.

14. Tazama, huyu ana utungu wa uovu,Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.

15. Amechimba shimo, amelichimba chini sana,Akatumbukia katika handaki aliyoifanya!

16. Madhara yake yatamrejea kichwani pake,Na dhuluma yake itamshukia utosini.

Zab. 7