Zab. 7:10-14 Swahili Union Version (SUV)

10. Ngao yangu ina Mungu,Awaokoaye wanyofu wa moyo.

11. Mungu ni mwamuzi mwenye haki,Naam, Mungu aghadhibikaye kila siku.

12. Mtu asiporejea ataunoa upanga wake;Ameupinda uta wake na kuuweka tayari;

13. Naye amemtengenezea silaha za kufisha,Akifanya mishale yake kuwa ya moto.

14. Tazama, huyu ana utungu wa uovu,Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.

Zab. 7