10. Ngao yangu ina Mungu,Awaokoaye wanyofu wa moyo.
11. Mungu ni mwamuzi mwenye haki,Naam, Mungu aghadhibikaye kila siku.
12. Mtu asiporejea ataunoa upanga wake;Ameupinda uta wake na kuuweka tayari;
13. Naye amemtengenezea silaha za kufisha,Akifanya mishale yake kuwa ya moto.
14. Tazama, huyu ana utungu wa uovu,Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.