21. Wakanipa uchungu kuwa chakula changu;Nami nilipokuwa na kiu wakaninywesha siki.
22. Meza yao mbele yao na iwe mtego;Naam, wakiwa salama na iwe tanzi.
23. Macho yao yatiwe giza wasione,Na viuno vyao uvitetemeshe daima.
24. Uimwage ghadhabu yako juu yao,Na ukali wa hasira yako uwapate.
25. Matuo yao na yawe ukiwa,Pasiwe na mtu wa kukaa hemani mwao.
26. Maana wanamwudhi mtu uliyempiga Wewe,Wanasimulia maumivu ya hao uliowatia jeraha.
27. Uwaongezee uovu juu ya uovu,Wala wasiingie katika haki yako.
28. Na wafutwe katika chuo cha uhai,Wala pamoja na wenye haki wasiandikwe.
29. Nami niliye maskini na mtu wa huzuni,Mungu, wokovu wako utaniinua.
30. Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo,Nami nitamtukuza kwa shukrani.
31. Nayo yatampendeza BWANA kuliko ng’ombe,Au ndama mwenye pembe na kwato.
32. Walioonewa watakapoona watafurahi;Enyi mmtafutao Mungu, mioyo yenu ihuishwe.
33. Kwa kuwa BWANA huwasikia wahitaji,Wala hawadharau wafungwa wake.