8. Nchi ilitetemekaNaam, mbingu zilidondoka usoni pa Mungu;Hata Sinai usoni pa Mungu; Mungu wa Israeli.
9. Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema;Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.
10. Kabila yako ilifanya kao lake huko;Ee Mungu, kwa wema wako uliwaruzuku walioonewa.
11. Bwana analitoa neno lake;Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;
12. Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia;Na mwanamke akaaye nyumbani agawa nyara.
13. Kwa nini kulala mazizini arukapo hua,Mbawa zake ziking’aa kama fedhaNa manyoya yake kama dhahabu?
14. Mwenyezi Mungu alipotawanya wafalme huko,Kulinyesha theluji katika Salmoni.