6. Mungu huwakalisha wapweke nyumbani;Huwatoa wafungwa wakae hali ya kufanikiwa;Bali wakaidi hukaa katika nchi kavu.
7. Ee Mungu, ulipotoka mbele ya watu wako,Ulipopita nyikani,
8. Nchi ilitetemekaNaam, mbingu zilidondoka usoni pa Mungu;Hata Sinai usoni pa Mungu; Mungu wa Israeli.
9. Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema;Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.
10. Kabila yako ilifanya kao lake huko;Ee Mungu, kwa wema wako uliwaruzuku walioonewa.
11. Bwana analitoa neno lake;Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;
12. Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia;Na mwanamke akaaye nyumbani agawa nyara.
13. Kwa nini kulala mazizini arukapo hua,Mbawa zake ziking’aa kama fedhaNa manyoya yake kama dhahabu?
14. Mwenyezi Mungu alipotawanya wafalme huko,Kulinyesha theluji katika Salmoni.
15. Ni mlima wa Mungu mlima Bashani,Ni mlima mrefu mlima Bashani.