19. Na ahimidiwe Bwana,Siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu;Mungu ndiye wokovu wetu.
20. Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa;Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA Bwana.
21. Naam, Mungu atakipasua kichwa cha adui zake,Utosi wenye nywele wa mtu afulizaye kukosa.
22. Bwana alisema, Kutoka Bashani nitawarudisha,Nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari;
23. Uuchovye mguu wako katika damu ya adui zako,Na ulimi wa mbwa zako upate sehemu yake.
24. Ee Mungu, wameiona miendo yako;Miendo ya Mungu wangu, Mfalme wangu, katika patakatifu
25. Waimbaji hutangulia, nyuma yao wapigao vinanda,Kati ya wanawali wapiga matari.
26. Mhimidini Mungu katika mikutano,Bwana katika makusanyiko ya Israeli.
27. Yuko Benyamini mdogo, mtawala wao;Wakuu wa Yuda, kundi lao;Wakuu wa Zabuloni;Wakuu wa Naftali.
28. Ee Mungu, uziamuru nguvu zako;Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu.
29. Kwa ajili ya hekalu lako YerusalemuWafalme watakuletea hedaya.
30. Mkemee mnyama wa manyasini;Kundi la mafahali, na ndama za watu;Hata wanyenyekee na kuleta vipande vya fedha,Uwatawanye watu wapendao vita.
31. Masheki watakuja kutoka Misri,Kushi itamnyoshea Mungu mikono yake mara.
32. Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu,Msifuni Bwana kwa nyimbo.
33. Apandaye mbingu za mbingu za tangu milele;Aitoa sauti yake, sauti ya nguvu.
34. Mhesabieni Mungu nguvu;Enzi yake i juu ya Israeli;Na nguvu zake zi mawinguni.