Zab. 66:6-11 Swahili Union Version (SUV)

6. Aligeuza bahari ikawa nchi kavu;Katika mto walivuka kwa miguu;Huko ndiko mlikomfurahia.

7. Atawala kwa uweza wake milele;Macho yake yanaangalia mataifa;Waasio wasijitukuze nafsi zao.

8. Enyi mataifa, mtukuzeni Mungu wetu,Itangazeni sauti ya sifa zake;

9. Aliyeiweka nafsi yetu katika uhai,Wala hakuuacha mguu wetu usogezwe.

10. Kwa maana umetupima, Ee Mungu,Umetujaribu inavyojaribiwa fedha.

11. Ulituingiza ndani ya wavu,Na kuweka viunoni mwetu mzigo uliotulemea.

Zab. 66