4. Nchi yote itakusujudia na kukuimbia,Naam, italiimbia jina lako.
5. Njoni yatazameni matendo ya Mungu;Hutisha kwa mambo awatendayo wanadamu;
6. Aligeuza bahari ikawa nchi kavu;Katika mto walivuka kwa miguu;Huko ndiko mlikomfurahia.
7. Atawala kwa uweza wake milele;Macho yake yanaangalia mataifa;Waasio wasijitukuze nafsi zao.
8. Enyi mataifa, mtukuzeni Mungu wetu,Itangazeni sauti ya sifa zake;