Zab. 64:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Mungu, uisikie sauti yangu katika malalamiko yangu;Unilinde uhai wangu na hofu ya adui.

2. Utanificha mbali na shauri la siri la watenda mabaya,Mbali na ghasia ya watu wafanyao maovu;

3. Waliounoa ulimi wao kama upanga,Wameielekeza mishale yao, maneno ya uchungu,

4. Wapate kumpiga mkamilifu faraghani,Kwa ghafula humpiga wala hawaogopi.

5. Walijifanya hodari katika jambo baya;Hushauriana juu ya kutega mitego;Husema, Ni nani atakayeiona?

Zab. 64