1. Ee Mungu wangu, uniponye na adui zangu,Uniinue juu yao wanaoshindana nami.
2. Uniponye nao wafanyao maovu,Uniokoe na watu wa damu.
3. Kwa maana wanaiotea nafsi yangu;Wenye nguvu wamenikusanyikia;Ee BWANA, si kwa kosa langu,Wala si kwa hatia yangu.