Zab. 59:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Ee Mungu wangu, uniponye na adui zangu,Uniinue juu yao wanaoshindana nami.

2. Uniponye nao wafanyao maovu,Uniokoe na watu wa damu.

3. Kwa maana wanaiotea nafsi yangu;Wenye nguvu wamenikusanyikia;Ee BWANA, si kwa kosa langu,Wala si kwa hatia yangu.

Zab. 59