6. Nikasema, Ningekuwa na mbawa kama njiwa,Ningerukia mbali na kustarehe.
7. Ningekwenda zangu mbali,Ningetua jangwani.
8. Ningefanya haraka kuzikimbiaDhoruba na tufani.
9. Ee Bwana, uwaangamize, uzichafue ndimi zao,Maana nimeona dhuluma na fitina katika mji.
10. Mchana na usiku huzunguka kutani mwake;Uovu na taabu zimo ndani yake;
11. Tamaa mbaya zimo ndani yake;Dhuluma na hila haziondoki mitaani mwake.