Zab. 55:4-8 Swahili Union Version (SUV)

4. Moyo wangu unaumia ndani yangu,Na hofu za mauti zimeniangukia.

5. Hofu na tetemeko limenijia,Na hofu kubwa imenifunikiza.

6. Nikasema, Ningekuwa na mbawa kama njiwa,Ningerukia mbali na kustarehe.

7. Ningekwenda zangu mbali,Ningetua jangwani.

8. Ningefanya haraka kuzikimbiaDhoruba na tufani.

Zab. 55