Zab. 55:16-20 Swahili Union Version (SUV)

16. Nami nitamwita Mungu,Na BWANA ataniokoa;

17. Jioni, asubuhi, na adhuhuri nitalalama na kuugua,Naye ataisikia sauti yangu.

18. Ameiokoa nafsi yangu iwe salama, asinikaribie mtu,Maana walioshindana nami walikuwa wengi.

19. Mungu atasikia na kuwajibu;Ndiye Yeye akaaye tangu milele.Mageuzi ya mambo hayawapati hao,Kwa hiyo hawamchi Mungu.

20. Amenyosha mkono awadhuru waliopatana naye,Amelihalifu agano lake.

Zab. 55