12. Kwa maana aliyetukana si adui;Kama ndivyo, ningevumilia.Aliyejitukuza juu yangu siye anichukiaye;Kama ndivyo, ningejificha asinione.
13. Bali ni wewe, mtu mwenzangu,Rafiki yangu, niliyejuana nawe sana.
14. Tulipeana shauri tamu; na kutembeaNyumbani mwa Mungu pamoja na mkutano.
15. Mauti na iwapate kwa ghafula,Na washuke kuzimu wangali hai,Maana uovu u makaoni mwao na katikati yao.