10. Mchana na usiku huzunguka kutani mwake;Uovu na taabu zimo ndani yake;
11. Tamaa mbaya zimo ndani yake;Dhuluma na hila haziondoki mitaani mwake.
12. Kwa maana aliyetukana si adui;Kama ndivyo, ningevumilia.Aliyejitukuza juu yangu siye anichukiaye;Kama ndivyo, ningejificha asinione.
13. Bali ni wewe, mtu mwenzangu,Rafiki yangu, niliyejuana nawe sana.
14. Tulipeana shauri tamu; na kutembeaNyumbani mwa Mungu pamoja na mkutano.
15. Mauti na iwapate kwa ghafula,Na washuke kuzimu wangali hai,Maana uovu u makaoni mwao na katikati yao.
16. Nami nitamwita Mungu,Na BWANA ataniokoa;
17. Jioni, asubuhi, na adhuhuri nitalalama na kuugua,Naye ataisikia sauti yangu.
18. Ameiokoa nafsi yangu iwe salama, asinikaribie mtu,Maana walioshindana nami walikuwa wengi.
19. Mungu atasikia na kuwajibu;Ndiye Yeye akaaye tangu milele.Mageuzi ya mambo hayawapati hao,Kwa hiyo hawamchi Mungu.