8. Unifanye kusikia furaha na shangwe,Mifupa uliyoiponda ifurahi.
9. Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu;Uzifute hatia zangu zote.
10. Ee Mungu, uniumbie moyo safi,Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu
11. Usinitenge na uso wako,Wala roho yako mtakatifu usiniondolee.
12. Unirudishie furaha ya wokovu wako;Unitegemeze kwa roho ya wepesi.
13. Nitawafundisha wakosaji njia zako,Na wenye dhambi watarejea kwako.
14. Ee MUNGU, Mungu wa wokovu wangu,Uniponye na damu za watu,Na ulimi wangu utaiimba haki yako.
15. Ee Bwana, uifumbue midomo yangu,Na kinywa changu kitazinena sifa zako.
16. Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa,Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.
17. Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika;Moyo uliovunjika na kupondeka,Ee Mungu, hutaudharau.