Zab. 50:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Mungu, Mungu BWANA, amenena, ameiita nchi,Toka maawio ya jua hata machweo yake.

2. Tokea Sayuni, ukamilifu wa uzuri,Mungu amemulika.

3. Mungu wetu atakuja wala hatanyamaza,Moto utakula mbele zake,na tufani yavuma sana ikimzunguka pande zote.

4. Ataziita mbingu zilizo juu,Na nchi pia awahukumu watu wake.

Zab. 50