Zab. 49:15-19 Swahili Union Version (SUV)

15. Bali Mungu atanikomboa nafsi yangu,Atanitoa mkononi mwa kuzimu, maana atanikaribisha.

16. Usiogope mtu atakapopata utajiri,Na fahari ya nyumba yake itakapozidi.

17. Maana atakapokufa hatachukua cho chote;Utukufu wake hautashuka ukimfuata.

18. Ajapojibariki nafsi yake alipokuwa hai,Na watu watakusifu ukijitendea mema,

19. Atakwenda kwenye kizazi cha baba zakeHawataona nuru hata milele.

Zab. 49