Zab. 47:4-8 Swahili Union Version (SUV)

4. Atatuchagulia urithi wetu,Fahari ya Yakobo ambaye alimpenda.

5. Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,BWANA kwa sauti ya baragumu.

6. Mwimbieni Mungu, naam, imbeni;Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni.

7. Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote,Imbeni kwa akili.

8. Mungu awamiliki mataifa,Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu.

Zab. 47