Zab. 47:3-8 Swahili Union Version (SUV)

3. Atawatiisha watu wa nchi chini yetu,Na mataifa chini ya miguu yetu.

4. Atatuchagulia urithi wetu,Fahari ya Yakobo ambaye alimpenda.

5. Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,BWANA kwa sauti ya baragumu.

6. Mwimbieni Mungu, naam, imbeni;Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni.

7. Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote,Imbeni kwa akili.

8. Mungu awamiliki mataifa,Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu.

Zab. 47