Zab. 40:5-9 Swahili Union Version (SUV)

5. Ee BWANA, Mungu wangu, umefanya kwa wingiMiujiza yako na mawazo yako kwetu;Hakuna awezaye kufananishwa nawe;Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri,Ni mengi sana hayahesabiki.

6. Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,Masikio yangu umeyazibua,Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.

7. Ndipo niliposema, Tazama nimekuja,(Katika gombo la chuo nimeandikiwa,)

8. Kuyafanya mapenzi yako,Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu;Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.

9. Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa.Sikuizuia midomo yangu; Ee BWANA, unajua.

Zab. 40