1. Nalimngoja BWANA kwa saburi,Akaniinamia akakisikia kilio changu.
2. Akanipandisha toka shimo la uharibifu,Toka udongo wa utelezi;Akaisimamisha miguu yangu mwambani,Akaziimarisha hatua zangu.
3. Akatia wimbo mpya kinywani mwangu,Ndio sifa zake Mungu wetu.Wengi wataona na kuogopa,Nao watamtumaini BWANA