1. Nalisema, Nitazitunza njia zanguNisije nikakosa kwa ulimi wangu;Nitajitia lijamu kinywani,Maadamu mtu mbaya yupo mbele yangu.
2. Nalikuwa sisemi, nalinyamaa kimya,Sina faraja, maumivu yangu yakazidi.
3. Moyo wangu ukawa moto ndani yangu,Na katika kuwaza kwangu moto ukawaka;Nalisema kwa ulimi wangu,
4. BWANA, unijulishe mwisho wangu,Na kiasi cha siku zangu ni kiasi gani;Nijue jinsi nilivyo dhaifu.
5. Tazama, umefanya siku zangu kuwa mashubiri;Maisha yangu ni kama si kitu mbele zako.Kila mwanadamu, ingawa amesitawi, ni ubatili.
6. Binadamu huenda tu huko na huko kama kivuli;Hufanya ghasia tu kwa ajili ya ubatili;Huweka akiba wala hajui ni nani atakayeichukua.
7. Na sasa ninangoja nini, Ee Bwana?Matumaini yangu ni kwako.