5. Jeraha zangu zinanuka, zimeoza,Kwa sababu ya upumbavu wangu.
6. Nimepindika na kuinama sana,Mchana kutwa nimekwenda nikihuzunika.
7. Maana viuno vyangu vimejaa homa,Wala hamna uzima katika mwili wangu.
8. Nimedhoofika na kuchubuka sana,Nimeugua kwa fadhaa ya moyo wangu.
9. Bwana, haja zangu zote ziko mbele zako,Kuugua kwangu hakukusitirika kwako.
10. Moyo wangu unapwita-pwita,Nguvu zangu zimeniacha;Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka.
11. Wanipendao na rafiki zangu wanasimama mbali na pigo langu;Naam, karibu zangu wamesimama mbali.
12. Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego;Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya;Na kufikiri hila mchana kutwa.