4. Maana dhambi zangu zimenifunikiza kichwa,Kama mzigo mzito zimenilemea mno.
5. Jeraha zangu zinanuka, zimeoza,Kwa sababu ya upumbavu wangu.
6. Nimepindika na kuinama sana,Mchana kutwa nimekwenda nikihuzunika.
7. Maana viuno vyangu vimejaa homa,Wala hamna uzima katika mwili wangu.
8. Nimedhoofika na kuchubuka sana,Nimeugua kwa fadhaa ya moyo wangu.