Zab. 38:10-14 Swahili Union Version (SUV)

10. Moyo wangu unapwita-pwita,Nguvu zangu zimeniacha;Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka.

11. Wanipendao na rafiki zangu wanasimama mbali na pigo langu;Naam, karibu zangu wamesimama mbali.

12. Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego;Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya;Na kufikiri hila mchana kutwa.

13. Lakini kama kiziwi sisikii,Nami ni kama bubu asiyefumbua kinywa chake.

14. Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,Ambaye hamna hoja kinywani mwake.

Zab. 38