10. Moyo wangu unapwita-pwita,Nguvu zangu zimeniacha;Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka.
11. Wanipendao na rafiki zangu wanasimama mbali na pigo langu;Naam, karibu zangu wamesimama mbali.
12. Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego;Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya;Na kufikiri hila mchana kutwa.
13. Lakini kama kiziwi sisikii,Nami ni kama bubu asiyefumbua kinywa chake.
14. Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,Ambaye hamna hoja kinywani mwake.