1. Ee BWANA, usinilaumu katika ghadhabu yako,Wala usiniadhibu kwa ukali wa hasira yako.
2. Kwa maana mishale yako imenichoma,Na mkono wako umenipata.
3. Hamna uzima katika mwili wanguKwa sababu ya ghadhabu yako.Wala hamna amani mifupani mwanguKwa sababu ya hatia zangu.
4. Maana dhambi zangu zimenifunikiza kichwa,Kama mzigo mzito zimenilemea mno.
5. Jeraha zangu zinanuka, zimeoza,Kwa sababu ya upumbavu wangu.
6. Nimepindika na kuinama sana,Mchana kutwa nimekwenda nikihuzunika.