1. Ee BWANA, usinilaumu katika ghadhabu yako,Wala usiniadhibu kwa ukali wa hasira yako.
2. Kwa maana mishale yako imenichoma,Na mkono wako umenipata.
3. Hamna uzima katika mwili wanguKwa sababu ya ghadhabu yako.Wala hamna amani mifupani mwanguKwa sababu ya hatia zangu.