24. Ajapojikwaa hataanguka chini,BWANA humshika mkono na kumtegemeza.
25. Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee,Lakini sijamwona mwenye haki ameachwaWala mzao wake akiomba chakula.
26. Mchana kutwa hufadhili na kukopesha,Na mzao wake hubarikiwa.
27. Jiepue na uovu, utende mema,Na kukaa hata milele.
28. Kwa kuwa BWANA hupenda haki,Wala hawaachi watauwa wake.Wao hulindwa milele,Bali mzao wa wasio haki ataharibiwa.
29. Wenye haki watairithi nchi,Nao watakaa humo milele.
30. Kinywa chake mwenye haki hunena hekima,Na ulimi wake husema hukumu.
31. Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake.Hatua zake hazitelezi.
32. Mtu asiye haki humvizia mwenye haki,Na kutafuta jinsi ya kumfisha.
33. BWANA hatamwacha mkononi mwake,Wala hatamlaumu atakapohukumiwa.
34. Wewe umngoje BWANA,Uishike njia yake,Naye atakutukuza uirithi nchi,Wasio haki watakapoharibiwa utawaona.
35. Nimemwona mtu asiye haki mkali sana,Akijieneza kama mwerezi wa Lebanoni.
36. Nikapita na kumbe! Hayuko,Nikamtafuta wala hakuonekana.