Zab. 37:15-18 Swahili Union Version (SUV)

15. Upanga wao utaingia mioyoni mwao wenyewe,Na nyuta zao zitavunjika.

16. Kidogo alicho nacho mwenye haki ni boraKuliko wingi wa mali wa wasio haki wengi.

17. Maana mikono ya wasio haki itavunjika,Bali BWANA huwategemeza wenye haki.

18. BWANA anazijua siku za wakamilifu,Na urithi wao utakuwa wa milele.

Zab. 37