Zab. 34:9-12 Swahili Union Version (SUV)

9. Mcheni BWANA, enyi watakatifu wake,Yaani, wamchao hawahitaji kitu.

10. Wana-simba hutindikiwa, huona njaa;Bali wamtafutao BWANA hawatahitaji kitu cho chote kilicho chema.

11. Njoni, enyi wana, mnisikilize,Nami nitawafundisha kumcha BWANA.

12. Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima,Apendaye siku nyingi apate kuona mema?

Zab. 34