9. Mcheni BWANA, enyi watakatifu wake,Yaani, wamchao hawahitaji kitu.
10. Wana-simba hutindikiwa, huona njaa;Bali wamtafutao BWANA hawatahitaji kitu cho chote kilicho chema.
11. Njoni, enyi wana, mnisikilize,Nami nitawafundisha kumcha BWANA.
12. Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima,Apendaye siku nyingi apate kuona mema?