4. Nalimtafuta BWANA akanijibu,Akaniponya na hofu zangu zote.
5. Wakamwelekea macho wakatiwa nuru,Wala nyuso zao hazitaona haya.
6. Maskini huyu aliita, BWANA akasikia,Akamwokoa na taabu zake zote.
7. Malaika wa BWANA hufanya kituo,Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.
8. Onjeni mwone ya kuwa BWANA yu mwema;Heri mtu yule anayemtumaini.
9. Mcheni BWANA, enyi watakatifu wake,Yaani, wamchao hawahitaji kitu.
10. Wana-simba hutindikiwa, huona njaa;Bali wamtafutao BWANA hawatahitaji kitu cho chote kilicho chema.
11. Njoni, enyi wana, mnisikilize,Nami nitawafundisha kumcha BWANA.