3. Mwimbieni wimbo mpya,Pigeni kwa ustadi kwa sauti ya shangwe.
4. Kwa kuwa neno la BWANA lina adili,Na kazi yake yote huitenda kwa uaminifu.
5. Huzipenda haki na hukumu,Nchi imejaa fadhili za BWANA.
6. Kwa neno la BWANA mbingu zilifanyika,Na jeshi lake lote kwa pumzi ya kinywa chake.
7. Hukusanya maji ya bahari chungu chungu,Huviweka vilindi katika ghala.
8. Nchi yote na imwogope BWANA,Wote wakaao duniani na wamche.