Zab. 33:18-21 Swahili Union Version (SUV)

18. Tazama, jicho la BWANA li kwao wamchao,Wazingojeao fadhili zake.

19. Yeye huwaponya nafsi zao na mauti,Na kuwahuisha wakati wa njaa.

20. Nafsi zetu zinamngoja BWANA;Yeye ndiye msaada wetu na ngao yetu.

21. Maana mioyo yetu itamfurahia,Kwa kuwa tumelitumainia jina lake takatifu.

Zab. 33