Zab. 27:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. BWANA ni nuru yangu na wokovu wangu,Nimwogope nani?BWANA ni ngome ya uzima wangu,Nimhofu nani?

2. Watenda mabaya waliponikaribia,Wanile nyama yangu,Watesi wangu na adui zangu,Walijikwaa wakaanguka.

3. Jeshi lijapojipanga kupigana nami,Moyo wangu hautaogopa.Vita vijaponitokea,Hata hapo nitatumaini.

Zab. 27