7. Wote wanionao hunicheka sana,Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao;
8. Husema, Umtegemee BWANA; na amponye;Na amwokoe sasa, maana apendezwa naye.
9. Naam, Wewe ndiwe uliyenitoa tumboni,Ulinitumainisha matitini mwa mama yangu.
10. Kwako nalitupwa tangu tumboni,Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu.
11. Usiwe mbali nami maana taabu i karibu,Kwa maana hakuna msaidizi.
12. Mafahali wengi wamenizunguka,Walio hodari wa Bashani wamenisonga;
13. Wananifumbulia vinywa vyao,Kama simba apapuraye na kunguruma.
14. Nimemwagika kama maji,Mifupa yangu yote imeteguka,Moyo wangu umekuwa kama nta,Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu.
15. Nguvu zangu zimekauka kama gae,Ulimi wangu waambatana na taya zangu;Unaniweka katika mavumbi ya mauti
16. Kwa maana mbwa wamenizunguka;Kusanyiko la waovu wamenisonga;Wamenizua mikono na miguu.
17. Naweza kuihesabu mifupa yangu yote;Wao wananitazama na kunikodolea macho.
18. Wanagawanya nguo zangu,Na vazi langu wanalipigia kura.
19. Nawe, BWANA, usiwe mbali,Ee Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia.