25. Kwako zinatoka sifa zanguKatika kusanyiko kubwa.Nitaziondoa nadhiri zanguMbele yao wamchao.
26. Wapole watakula na kushiba,Wamtafutao BWANA watamsifu;Mioyo yenu na iishi milele.
27. Miisho yote ya dunia itakumbuka,Na watu watamrejea BWANA;Jamaa zote za mataifa watamsujudia.
28. Maana ufalme una BWANA,Naye ndiye awatawalaye mataifa.
29. Wakwasi wote wa dunia watakula na kusujudu,Humwinamia wote washukao mavumbini;Naam, yeye asiyeweza kujihuisha nafsi yake,
30. Wazao wake watamtumikia.Zitasimuliwa habari za BWANA,Kwa kizazi kitakachokuja,