Zab. 22:25-30 Swahili Union Version (SUV)

25. Kwako zinatoka sifa zanguKatika kusanyiko kubwa.Nitaziondoa nadhiri zanguMbele yao wamchao.

26. Wapole watakula na kushiba,Wamtafutao BWANA watamsifu;Mioyo yenu na iishi milele.

27. Miisho yote ya dunia itakumbuka,Na watu watamrejea BWANA;Jamaa zote za mataifa watamsujudia.

28. Maana ufalme una BWANA,Naye ndiye awatawalaye mataifa.

29. Wakwasi wote wa dunia watakula na kusujudu,Humwinamia wote washukao mavumbini;Naam, yeye asiyeweza kujihuisha nafsi yake,

30. Wazao wake watamtumikia.Zitasimuliwa habari za BWANA,Kwa kizazi kitakachokuja,

Zab. 22