23. Ninyi mnaomcha BWANA, msifuni,Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo, mtukuzeni,Mcheni, enyi nyote mlio wazao wa Israeli.
24. Maana hakulidharau teso la mteswa,Wala hakuchukizwa nalo;Wala hakumficha uso wake,Bali alipomlilia akamsikia.
25. Kwako zinatoka sifa zanguKatika kusanyiko kubwa.Nitaziondoa nadhiri zanguMbele yao wamchao.
26. Wapole watakula na kushiba,Wamtafutao BWANA watamsifu;Mioyo yenu na iishi milele.
27. Miisho yote ya dunia itakumbuka,Na watu watamrejea BWANA;Jamaa zote za mataifa watamsujudia.