22. Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu,Katikati ya kusanyiko nitakusifu.
23. Ninyi mnaomcha BWANA, msifuni,Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo, mtukuzeni,Mcheni, enyi nyote mlio wazao wa Israeli.
24. Maana hakulidharau teso la mteswa,Wala hakuchukizwa nalo;Wala hakumficha uso wake,Bali alipomlilia akamsikia.
25. Kwako zinatoka sifa zanguKatika kusanyiko kubwa.Nitaziondoa nadhiri zanguMbele yao wamchao.