16. Kwa maana mbwa wamenizunguka;Kusanyiko la waovu wamenisonga;Wamenizua mikono na miguu.
17. Naweza kuihesabu mifupa yangu yote;Wao wananitazama na kunikodolea macho.
18. Wanagawanya nguo zangu,Na vazi langu wanalipigia kura.
19. Nawe, BWANA, usiwe mbali,Ee Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia.
20. Uniponye nafsi yangu na upanga,Mpenzi wangu na nguvu za mbwa.
21. Kinywani mwa simba uniokoe;Naam, toka pembe za nyati umenijibu.
22. Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu,Katikati ya kusanyiko nitakusifu.