Zab. 17:7-11 Swahili Union Version (SUV)

7. Dhihirisha fadhili zako za ajabuWewe uwaokoaye wanaokukimbilia;Kwa mkono wako wa kuumeUwaokoe nao wanaowaondokea.

8. Unilinde kama mboni ya jicho,Unifiche chini ya uvuli wa mbawa zako;

9. Wasinione wasio haki wanaonionea,Adui za roho yangu wanaonizunguka.

10. Wameukaza moyo wako,Kwa vinywa vyao hutoa majivuno.

11. Sasa wametuzunguka hatua zetu,Na kuyakaza macho yao watuangushe chini.

Zab. 17