1. Mungu, unihifadhi mimi,Kwa maana nakukimbilia Wewe.
2. Nimemwambia BWANA, Ndiwe BWANA wangu;Sina wema ila utokao kwako.
3. Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora,Hao ndio niliopendezwa nao.
4. Huzuni zao zitaongezekaWambadilio Mungu kwa mwingine;Sitazimimina sadaka zao za damu,Wala kuyataja majina yao midomoni mwangu.
5. BWANA ndiye fungu la posho langu,Na la kikombe changu;Wewe unaishika kura yangu.
6. Kamba zangu zimeniangukia mahali pema,Naam, nimepata urithi mzuri.
7. Nitamhimidi BWANA aliyenipa shauri,Naam, mtima wangu umenifundisha usiku.