Zab. 16:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Mungu, unihifadhi mimi,Kwa maana nakukimbilia Wewe.

2. Nimemwambia BWANA, Ndiwe BWANA wangu;Sina wema ila utokao kwako.

3. Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora,Hao ndio niliopendezwa nao.

4. Huzuni zao zitaongezekaWambadilio Mungu kwa mwingine;Sitazimimina sadaka zao za damu,Wala kuyataja majina yao midomoni mwangu.

5. BWANA ndiye fungu la posho langu,Na la kikombe changu;Wewe unaishika kura yangu.

6. Kamba zangu zimeniangukia mahali pema,Naam, nimepata urithi mzuri.

7. Nitamhimidi BWANA aliyenipa shauri,Naam, mtima wangu umenifundisha usiku.

Zab. 16