Zab. 147:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Haleluya.Msifuni Bwana;Maana ni vema kumwimbia Mungu wetu,Maana kwapendeza, kusifu ni kuzuri.

2. BWANA ndiye aijengaye Yerusalemu,Huwakusanya waliotawanyika wa Israeli.

3. Huwaponya waliopondeka moyo,Na kuziganga jeraha zao.

4. Huihesabu idadi ya nyota,Huzipa zote majina.

5. Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu,Akili zake hazina mpaka.

6. BWANA huwategemeza wenye upole,Huwaangusha chini wenye jeuri.

7. Mwimbieni BWANA kwa kushukuru,Mwimbieni Mungu wetu kwa kinubi.

Zab. 147